Haki miliki ya pichaAFP
Image captionImage result for VITA IRAQ WATOTO WA TESEKAVita nchini Iraq, vimewaathiri zaidi wanawake na watoto
Shirika la Kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF limeonya kwamba watoto takriban milioni tano nchini Iraq wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.
Shirika hilo limesema watoto wa nchi hiyo hususan wale wote walio katika mji wa Mosul, ambako majeshi ya Iraq yanapambana vikali na wapiganaji wa Islamic state, wamejikuta katika ghasia na umasikini usio na mwisho.
Takwimu zilizooneshwa na UNICEF zinaonesha kuwa nusu ya wagonjwa wanaotibiwa katika vituo vya watu wenye maradhi ya wasiwasi na kuchanganyikiwa kutokana na hofu, (magonjwa mabaya ya akili) magharibi mwa Mosul ni watoto.
Kwa mujibu wa ripoti, watoto wapatao laki nane nchini Iraq kote, wamepoteza mzazi japo mmoja.
Mashirika ya misaada yanasema fedha zaidi zinahitajika haraka kuweza kusaidia kuwalinda watoto wa Iraq, kutokana na mapigano hayo.

KWAMATANGAZO YA BIASHARA KWAYA NYIMBO AINA ZOTE HABARI YEYOTE TUPIGIE   SASA KWA NUMBE,WHATSAPP FB //+255 623372368=+255768163863

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Chapisha Maoni

 
Top