HARMONISEHaki miliki ya pichaINSTAGRAM
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesema kuwa anatamani msanii wa muziki ,Rajab Abdul maarufu kama Harmonize au 'konde boy' kugombea nafasi ya ubunge katika jimbo la Tandahimba mkoani Mtwara, limeripoti gazeti la Mwananchi nchini Tanzania.
Rais Magufuli amesema hayo katika mkutano wa hadhara , mara baada ya msanii huyo kutumbuiza katika mkutano huo huko mkoani Lindi.
Harmonise amekuwa akikaribishwa kutumbuiza katika mikutano mbalimbali ya hadhara inayofanya rais Magufuli mara baada ya kutoa wimbo wake wa Magufuli.
Wimbo huo wa Magufuli ulioimbwa kwa mdundo wa nyimbo yake ya zamani ya kwangaru, umemsifu Magufuli kwa kazi aliyoifanya katika taifa hilo.
"I wish ningemuona Magufuli nimpigie magoti na kumpongeza hadharani...mchapakazi hachoki...Fly over sasa tunazo, Airport imeshajengwa...acha nikupongeze kwa Air Tanzania..."wimbo wa Harmonise unaoitwa Magufuli.
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Chapisha Maoni

 
Top