
Askari polisi akipiga bomu nyumbani kwa marehemu mwendesha bodaboda kusambaratisha waombolezaji leo Shinyanga-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog
Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limetumia mabomu ya machozi na maji ya kuwasha kuwasambaratisha waendesha bodaboda mjini Shinyanga waliokuwa wamefunga barabara kuu ya Shinyanga – Tabora wakidai askari wa jeshi hilo amesababisha kifo cha mwendesha bodaboda mwenzao

Askari polisi akipiga bomu nyumbani kwa marehemu mwendesha bodaboda kusambaratisha waombolezaji leo Shinyanga-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog
Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limetumia mabomu ya machozi na maji ya kuwasha kuwasambaratisha waendesha bodaboda mjini Shinyanga waliokuwa wamefunga barabara kuu ya Shinyanga – Tabora wakidai askari wa jeshi hilo amesababisha kifo cha mwendesha bodaboda mwenzao-
Mabomu ya machozi yameanza kupigwa leo Jumatano June 7,2017 tangu asubuhi mpaka majira ya saa sita mchana katika mitaa mbalimbali mjini Shinyanga.
Wakati polisi wakipiga mabomu,wananchi,waendesha bodaboda nao walikuwa wanajibu mashambulizi kwa kuwarushia mawe askari polisi.
Wakati polisi wakipiga mabomu,wananchi,waendesha bodaboda nao walikuwa wanajibu mashambulizi kwa kuwarushia mawe askari polisi.
Pamoja na jeshi hilo kupiga mabomu, limekwenda hadi nyumbani kwenye msiba alipokuwa akiishi marehemu na kuwatawanya kwa kuwakamata bodaboda na pikipiki zao hali iliyozua taharuki zaidi.
Inaelezwa kuwa waendesha bodaboda hao wamegoma kumzika mwenzao wakishinikiza mpaka mkuu wa mkoa afike nyumbani kwa marehemu.
TAARIFA ZAIDI TUTAENDELEA KUWALETEA HAPA HAPA MALUNDE1 BLOG

Gari la maji ya kuwasha likimwaga maji
TAARIFA ZAIDI TUTAENDELEA KUWALETEA HAPA HAPA MALUNDE1 BLOG

Gari la maji ya kuwasha likimwaga maji
Chapisha Maoni