Kurugenzi ya Sheria ya Mtandao wa Wanafunzi Tanzania TSNP imekusudia kuwasilisha kwa kampuni inayoandaa MISS TZ notisi ya madai na kusudio la kuwafikisha Mahakamani kama watashindwa kuwalipa washindi wa MISS TZ 2016.

Hatua hiyo inakuja baada ya Kurugenzi hiyo kupokea malalamiko kutoka kwa mamiss walioshiriki Miss Tanzania 2016 na kushinda nafasi za 2, 3 na 4 kutolipwa fedha zao walizoahidiwa na waandaaji wa mashindano hayo Lino International Agency Ltd.


TSNP imewataja washindi hao kuwa ni Mary Peter Clavery (Miss TZ 02), Grace Christopher Malikita (Miss TZ 03) na Anna Nitwa (Miss TZ 04) ambapo tayari mawakili wemepitia mikataba yao na kujiridhisha kuwa waandaaji wamekiuka.KWAMATANGAZO YA BIASHARA NYIMBO ZA ASILI,WASILIANA NASI;0623372368
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Chapisha Maoni

 
Top